facebook

Friday, December 13, 2013

NEW HIP HOP LOGO!

New HIP  HOP logo toka wapoteen click soon itakuwa mtaani! by G Rambo Wapoteen

Friday, November 15, 2013

LEO NI SIKU YA KUZALIWA KWA ADAM MILASI!

ADAM NA MARAFIKI

ADAM MILASI

ADAM MILASI

ADAM MILASI

ADAM NA MARAFIKI
HAPPY B DAY ADAM MILASI N LARGE LIFE FOR YOU!

Monday, October 21, 2013

LEO NI SIKU YA KUZALIWA KWA MWANA FAMILIA YA WAPOTEEN CLICK KIBABU WAPOTEEN!

KIBABU WAPOTEEN

KIBABU WAPOTEEN

KIBABU WAPOTEEN NA  MARAFIKI

CURTIS/MASHAKA / KAMANDA N MUBA JEMBE

KIBABU WAPOTEEN NA FAMILLY
FAMILIA YA WAPOTEEN CLICK ILIYOPO DAR ES SALAAM KIGOGO LUHANGA

INAFURAHA SANA SIKU YA LEO KWA KUWA MMOJA WA FAMILIA YETU ANATIMIZA MIAKA KAZAA NI #KIBABU WAPOTEEN

TUNA MTAKIA MAISHA MAREFU YENYE FURAHA SIKU ZOTE ZA MAISHA YAKE 

PIA ASISAHAU KUMSHUKURU MUNGU KWA KUMFIKISHA HADI HAPA ALIPOFIKA, PAMOJA NA KUWAHESHIMU WAZAZI WAKE...!!

Sunday, October 20, 2013

HILE MIXTAPE YA P THE MC MWINGI WA HABARI INAPATIKANA SASA!

P THE MC

 P the mc "mawenge", mwingi wa habari ndo mpango mzima copy buku 5, piga 0717254451, 0713659043, 0712229229, 0655017116. by wapoteen click!

Wednesday, October 9, 2013

Historia ya DUKE TACHEZ: katika safari yake ya u-producer!

DUKE
 Anajulikana zaidi kwa jina la DUKE TACHEZ lakini jina lake halisi ni Duke Gervalius Duke. Alianza kufanya kazi ya kutengeneza Music mwaka 1998 akiwa mtaani tu. Kwa sababu kipindi iko ilikua ni vigumu kuingia kwenye studio kubwa kama Bongo Records.
Duke Tachez alipendelea sana kutengeneza midundo aina ya Hip Hop, na Mwaka 2002 alifanikiwa kuingia kwenye studio Dynamic grooves ambayo alikuwa akishare na rafiki. Ambayo haikujulikana sana kwa sababu ya kufanya kazi nyingi za Undergrounds.

Mwaka 2004 baada ya studio kuanzishwa ambayo ilikua ikiitwa Pinnacle Production wakiwa na producer kutoka kenya Dunga na wakafanikiwa kufanya kazi kama Usipime ya Black Rinno, Temba Ft Ray C – Nipe Mimi, Profesa ft Bamboo – Karibu, Chegge ft Temba – Hili Dude na nyingine nyingi.
Duke hakuishia hapo tu mwaka 2005-2008 akatoka Pinnacle production na akaamua kuwa Producer wa kujitegemea na alifanikiwa kufanya kazi na Studio mbali mbali kama 41 records, Kama Kawa Records, Pasu kwa Pasu records, Dhahabu Records, Bongo Records & Tongwe Records Ambapo alifanikiwa kufanya nyimbo ni ya Wanaume halisi – tatu bila Remix, I am Proffesinal ya Fid Q, Zero – Witness ft Fid Q, O-ten ft Chidi – Nyandindi, Chiku Ketto ft Lameck Ditto – Muda Umefika, Ripoti za Mtaani Fid Q ft Zahiri Zorro, Traveller ya Solo Thang, Babuu wa kitaa – Wa Kitaa.
Duke pia alifanikiwa kufanya Mixtape KITAANI VOL 1 ambayo ilikua na collection ya baadhi ya nyimbo ambazo aliwahi kufanya akiwa kwenye studio mbali mbali.

DUKE

Tuesday, September 10, 2013

SOMA HISTORIA YA STEREO B-BOY STEREO HAPA!

STEREO a.k.a B BOY STEREO 


Genre: Hip Hop

Ni tangu pale wimbo wa “nitabaki juu” ulivyoanza kusikika kwa hadhira ya Tanzania,stereo akitumia sanaa kuonyesha yeye ni nani.Stereo alianza kufuatilia Hip Hop tangu akiwa darasa la pili, mwaka 1998. Kwa kutambua kuwa ana kipaji cha kufanya Hip Hop mara baada ya kusikia ladha ya huu mziki… hatimaye alianza kuiga kuchana mistari ya emcees wengine wa Bongo, kama vile A.Y., Professor Jay, Complex (R.I.P.), Fid Q ,Solo Thang na Hasheem Dogo Mwendawazimu mpaka ughaibuni kwa kughani nyimbo za Talib Kweli .Xzibit, Jay Z, Notorious BIG, Coolio na Nas.

 Stereo alikutana na Nikki Mbishi shule ya msingi, ambapo waliendelea na huo mchezo wa kuimba nyimbo za wasanii wengine.Stereo anadai alianza rasmi kuandika lyrics zake mwenyewe akiwa darasa la nne… pamoja na Nikki.

Akiwa anaonyesha hisia zake kwa kutumia multi-syllable rhymes akipendelea kuokota maneno ya mitaani zaidi, kwa kiasi fulani, hasa yale adimu kama ‘kucheza ndondo’, ‘komando kipensi’, ‘buti lenye uvundo’, ‘msela nondo’, n.k. , mitambao ambayo wengi wanamfananisha na One The Incredible, ambaye pia anapendelea kutumia multi-syllable rhymes.Umoja wao na Nikki Mbishi aliyefanya stereo kupata deal la M-Lab umekuwa ni tochi ya kizazi kipya cha hip hop Tanzania.

Stereo anasomea “bachelor of science in urban and regional planning” huku akiendelea kushika mic na kuiwakilisha mtaa,kwa sasa Stereo yupo chini ya Unity Entertainment kampuni inayomilikiwa na A.y mkataba aliosaini mwishoni mwa mwaka 2012.


Top 5 emcees wa stereo kutoka Bongo, na kwanini?
Professor Jay, Fid Q, Nikki Mbishi, One The Incredible na Kurasa The Page. Jamaa wana mistari na flow kali sana. Sichoki kuwasikiliza kila siku sababu mistari yao inaishi. 

MHADHARA WA HIPHOP....MHADHARA WA HIP HOP....MHADHARA WA HIPHOP!

 

Kwa wale wakazi wa Bandari ya Salama zamani kuitwa MZIZIMA Ni fursa yenu na hii si ya kukosa,lakini mtajiuliza ni nini hiki? Utamaduni huu umekuja kupeana elimu/maarifa (knowledge) hivyo hatuna budi peana chakula hiki cha akili,Sasa soma hapa chini upate maelekezo. TAREHE: 13/09/2013 MUDA: 11:00 - 1:00 JIONI WAPI: ALLIANCE FRANCAISE KIINGILIO: BURE KABISA Wadau,wakereketwa wa utamaduni huu wote mnakaribishwa siku hiyo njoo ujifunze mengi kupitia ''MHADHARA HURU'' utakaotolewa na NASH EMCEE (Maalim),bila ajizi siku hiyo atatukumbusha na kutuelezea ni nini *Machata,*Wachenguaji*Wadundishaji,*Mavunjaji*Maarifa kwa wenye vipaji,

JIFUNZE MENGI KUHUSU HIPHOP


HIPHOP umekuwa ni utamaduni au nyenzo adhimu kabisa ambao unawaunganisha watu wa aina mbalimbali hapa duniani hasa kwa wale wanaoishi katika misingi yake,kwani mbali na kuburudisha hadhira yake,umekuwa ni utamaduni wa kuyaangazia mambombali katika jamii zetu kwa jicho ang'avu lisilo na shaka na kujaribu kutoa suluhu au kuchokoa mambo mbalimbali na kuwaacha watu wakiwa katika tafakuri la kipi wakifanye baada ya kuupata ukweli kupitia HIPHOP,thibitisha hili kwa kurejelea kibao cha ''NASH MC'' Kaka Suma na vingine vingi adhimu. Kila kitu kizuri huwa na changamoto nyingi mfano.ni hili watu wanaojiita WANAHIPHOP kutojifunza zaidi na kufata misingi ya utamaduni huu,hivyo ni wajibu wetu kujifunza ukweli na undani wake,

Tuesday, September 3, 2013

Monday, September 2, 2013

LEO NI SIKU YA KUZALIWA KWA MWANA FAMILIA YA WAPOTEEN CLICK KENY WAPOTEEN!

Keny Wapoteen
FAMILIA YA WAPOTEEN CLICK ILIYOPO DAR ES SALAAM KIGOGO LUHANGA

INAFURAHA SANA SIKU YA LEO KWA KUWA MMOJA WA FAMILIA YETU ANATIMIZA MIAKA KAZAA NI #KENY WAPOTEEN

TUNA MTAKIA MAISHA MAREFU YENYE FURAHA SIKU ZOTE ZA MAISHA YAKE

PIA ASISAHAU KUMSHUKURU MUNGU KWA KUMFIKISHA HADI HAPA ALIPOFIKA, PAMOJA NA KUWAHESHIMU WAZAZI WAKE...!!

Saturday, August 24, 2013