facebook

Friday, August 15, 2014

Picha: Adidas na FIFA wamkabidhi James Rodriguez mzigo wa dhahabu.

Shirikisho la soka duniani FIFA, hii leo limekabidhi tuzo ya mfungaji bora wa fainali za kombe la dunia zilizohitimishwa nchini Brazil July 13 mwaka huu, mshambuliaji kutoka nchini Colombia na klabu ya Real Madrid James David Rodríguez Rubio.
FIFA wamemkabidhi tuzo hiyo Rudriguez mwenye umri wa miaka 23, ambayo ni kiatu cha dhahabu mjini Madrid ikiwa ni sehemu ya kutimiza makabidhiano ya zawadi kwa washindi mbali mbali wa fainali wa kombe la dunia za mwaka 2014.
Rodríguez, amepokea tuzo hiyo ambayo imetolewa na kampuni ya vifaa vya michezo ya Adidas sambamba na tuzo nyingine ya bao bora la fainali za kombe la dunia mwaka 2014, ambalo alilifungwa wakati wa mchezo wa hatua ya 16 bora kati ya Colombia dhidi ya Uruguay.
Tuzo ya goli bora la fainali za kombe la dunia za mwaka huu aliyokabidhiwa James David Rodríguez Rubio, ni viatu vya Adidas vyenye mfano wa toleo la sasa ambavyo vimetengenezwa kwa madini ya dhahabu.






No comments:

Post a Comment