Rais wa Sudan Omar al-Bashir ametishia, kufunga kabisa bomba la mafuta
ambalo husafirisha mafuta kutoka Sudan Kusini hadi pwani ya Sudan, Red
Sea.
Alisema kuwa Sudan itasitisha usafirishwaji wa mafuta ikiwa Sudan
Kusini haitakoma kuwaunga mkono waasi wanaoendesha harakati zao katika
eneo la mafuta la Sudan.
Jeshi la Sudan linapambana na waasi katika angalao maeneo matatu ya nchi hiyo.
Licha ya Sudan Kusini kujitawala mwaka 2011, hali ya wasiwasi kuhusu mafuta na ardhi imekuwa ikiendelea.
''Na sasa natoa onyo la mwisho kwa ndugu zetu wa
Sudan Kusini kuwa tutafunga kabisa bomba la mafuta ikiwa wataendelea
kuunga mkono wasaliti katika jimbo la Darfur , Kordofan ya Kusini na
Blue Nile'' alisema Bashir kupitia televisheni ya taifa huku akigusia
waasi wanaoendesha harakati zao katika maeneo hayo.
Kundi la waasi lenye mirengo mingi,
linalojulikana kama Sudan Revolutionary Front (SRF), limefanya
mashambulizi katika miji kadhaa huku wakiteka mji mkubwa wa Um Rawaba ,
katikati mwa Sudan mwezi Aprili.
Kundi hilo linalonuia kuipindua serikali ya rais
Bashir, lakini wakaendelea kudhibiti mji wa Abu Kershola, katika eneo
jirani la Kordofan Kusini.
Waasi wa SPLM-North walijiunga na kundi la waasi
la JEM kutoka Darfur pamoja na makundi mengine ambayo ni ya mrengo wa
(SLA), kwa lengo la kubuni kundi la
Sudan Revolutionary Front mwaka jana.
Rais Bashir alitoa hotuba yake moja kwa moja
kupitia televisheni ya taifa nchini Sudan, kufuatia tangazo la jeshi
kuwa limeweza kuteka tena mji wa Abu Kershola kutoka kwa waasi.
Wakati huohuo, msemaji wa waasi hao aliambia
shirika la habari la AFP kuwa wapiganaji waliondoka kutoka, eneo la Abu
Kershola ili kulegeza vikwazo vya serikali kwa wenyeji wa eneo hilo.
Uhusiano kati ya nchi hizo mbili umekuwa ukitetereka tangu mwaka 2011, wakati Sudan Kusini ilipoamua kujitawala.
Maswala muhimu kuhusu Uzalishaji wa mafuta, mizozo ya mipaka ynagali kutatuliwa.
No comments:
Post a Comment